Kiama

Yesu aliwaahidi wanafunzi wake ya kuwa atarudi tena. Imeandikwa, Yohana 14:1-3 "Msifadhaike mioyoni mwenu mnamwanamini Mungu niamimini na mimi nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi kama sivyo ningaliwaambia maana naenda kuwaandalia mahali bai mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena ni wakaribishe kwangu ili nilipo nanyi muwepo."

Malaika waliahidi ya kuwa yesu atarudi tena. Imeandikwa, Matendo ya mitume 1:10-11 "Walipokuwa wakikaza macho mbinguni, yeye alipokuwa akienda zake, tazama watu wawili wakasimama karibu nao wenye nguo nyeupe waka sema enyi watu wa Galilaya mbona mmesimama mkitazama mbinguni huyu Yesu aliye chukuliwa kutoka kwenu kwanda juu mbinguni atakuja jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni."

Yesu atakujaje?. Imeandikwa, Luka 21:27 "Hapo ndipo watakapo mwona mwana wadamu akija katika wingu pamoj ana nguvu na utukufu mwingi."

Wangapi watamwona akija mara ya pili? Imeandikwa, Ufunuo 1:7 "Tzama yuaja na mawingu na kila jicho litamwona na hao waliomchoma na kabila zote za dunia wataomboleza kwa ajili yake naam amini."

Tuta ona nini na kusikia nini wakati Yesu atakaporudi.? Imeandikwa, 1Wathesalonike 4:16-17 "Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko na sauti ya malaika mkuu na parapanda ya Mungu na hao waliokufa kwanza watafufuliwa kwanza kisha sisi tulio hai, tuliosalia tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa na Bwana milele."

Je kuonekana kwake kutakuaje?. Imeandikwa, Mathayo 24:27 "Kwa maana kama vile umeme utokavyo mashariki ukaonekana hata magharibi, hivyo ndivyo kutakavyo kuwa kuja kwake mwana wa Adamu."

Je Mungu ametupa maonyo gani kuhusu kuja kwake tusije tukadanganyika?. Imeandikwa, Mathayo 24:23-26 "Wakati huo mtu akiwaambia tazama Kristo yupo hapa au yuko kule msisadiki kwamaana watatokea akristo wa uongo na manabii wa uongo nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza kama yamkini hata walio wateule tazama nimekwisha kuwaonya mbele basi wakiwaambia yuko jangwani msitoke yumo nyumbani msisadiki."

Je kuna mtu ajuae wakati wakuja kwake Yesu?. Imeandikwa, Mathayo 24:36 "Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye hata malaika walio mbinguni wala mwana ila Baba peke yake."

Wanadamu hupendaisha mambo je Kristo asema je. Imeandikwa, Mathoyo 24:42 "Kesheni basi, kwa maana hamjui ni siku ipi atakapokuja Bwana wenu."

Nionyo gani ambalo Kristo alitoa tusije tukakutwa bila ya kujiandaa. Imeandikwa, Luka 21:34-36 "Basi jiangalieni mioyo yenu isije ikalemewa na ulafi na ulevi na masumbufu ya maisha haya siku ile ikawajia ghafula kama mtego unasavyo kwa kuwa ndivyoitakavyo wajia watu wote wakaao juu ya uso wa dunia nzima Basi kesheni niyni kila wakati akiomba ili mpate kuokoka katika haya yote yatakayotokea ann kusimama bele za mwana wa Adamu."

Kwa nini kuja kwa Yesu kumekawia?. Imeandikwa, 2Petro 3:8-9 "Lakini wapenzi msilisahau neno hili kwamba kwa Bwana siku moja nikama miaka elfu na miak aelfu nikama siku moja Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake kama wengine wanvyo kudhani kukawia bali huvumilia kwenu maana hapendi mtu yo yote apotee bali wote wafikie toba."

Tunapo msubiri Yesu twapaswa kufanya nini? Imeandikwa Titu 2:11-14 "Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi na haki na utauwa katika ulimwengu huu wa sasa. Tukilitumainia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Yesu Mungu mkuu na mwokozi wetu amabye alitoa nafsi yake kwa ajili yetu ili atukomboe na maasi yote na kujisafishia watu wawe milki yake mwenyewe bwale walio na juhudi katika matendo mema."

Je! Ulimwengu utakuwaje wakati Yesu arudipo? Imeandikwa, Mathayo 24:37-39 "Kwa maana kama ilivyo uwa siku za nuhu ndivyo utakavyo kuja kwake mwana wa Adamu kwa kuwa kama vile siku zile zilizokuwa kabla ya garika watu walivyo kuwa wakila na kunywa wakioa na kuolewa hat siku ile aliyo ingia Nuhu katika safina wasitambue hata gharika ikaja ikawashukua wote ndivyo kutakavyokuwa kuja kwa mwana wa Adamu." Imeandikwa, Mathayo 16:27 na Ufunuo 22:12 "Kwa sababu wamawa Adamu atakuja kwa utukufu wa Baba yeke pamoja na malaika zake; ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake." Tazama naja upesi na ujira wangu upamoja nami kumlipa kila tu kama kazi yake ilivyo."

Kwa nini Yesu arudi tena?. Imeandikwa, Waebrania 9:28 "Kadhalika Kristo naye akisha kutolewa sadaka mara moja azichukue dhambi za watu wengi atatokea mara ya pili pasipo dhabi kwa haowatazamiao kwa wokovu."

Yesu atakapokuja ndipo tutasikia hali ya wokovu wetu. Imeandikwa, 1Wakorintho 1:7-8 "Hatahamkupungukia na karama yo yote mkikutazamia sana kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo amabaye atawadhibitisha hata mwisho ili msilaumiwe siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo."