Home / Masomo ya Biblia / Siku za mwisho

Siku za mwisho

Makafiri hawaamini yakuwa dunia inakaribia kisha na mwisho ukaribu. Imeandikwa 2Petero 3:3-4 "Mkijua kwanza neno hili ya kwamba katika siku za mwisho kutakuja na dhihaka za watu wenye kudhihaki wafuatao tamaa za wenyewe na kusema ikowapi ahadi ile ya kuja kwake kwa maana tangu hapo babu zetu walipolala vitu vyote vinakaa hali iyo hiyo tangu mwanzo wa kuumbwa."

Kuja kwa mpinga Kristo ni dalili ya mwisho wa dunia. imeandikwa, 1Yohana 2:18 "Watoto ni wakati wa mwisho na kama vilelivyosikia kwamba mpinga Kristo yuaja hata sasa wapinga Kristo wengi wamekwisha kuwapo kwa sababu hiyo twajua ni wakati wa mwisho."

Je! Yesu alisema jinsi mwisho utakavyo kuja?. Imeandikwa, Mathayo 24:14, "Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote kuwa ushuhuda kwa mataifa yote hapo ndipo ule mwisho utakapo kuja."

Watu watakuja kwa mfano wa yesu nao watapoteza wengi. Imeandikwa, Mathayo 24:23-24 "Wakati huo mtu akiwaambia tazama Kristo yupo hapa au yuko kule msisadiki. kwa maana watatoke makristo wa uongo nao watatoa ishara kubwa na maajabu wapate kuwapoteza kama yakini hata walio wateule."

Kutakuwa na ishra kaqtika mwezi jua na hata nyota. Imeandikwa, Mathayo 24:29-30 "Lakini mara baada ya dhiki ya siku zile jua litatiwa giza na mwezi hautatoa mwanga wake na nyota zitaanguka mbinguni na nguvu za mbingu zitatikisika. Ndipo itakapoonekana ishara ya mwan wa Adamu mbinguni; ndipo mataifa ya ulimwengu watakapoomboleza na watamwona mwana wa Adamu akija juu ya mawingu ya mbinguni pamoja na nguvu na utukufu mwingi."

Je! siku za mwisho zitakua vipi?. Imeandikwa, 2Timotheo 3:1-5 "Lakini ufahamu neno hili ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe wenye kupenda fedha wenye kujisifu wenye kiburi wenye kutukana wasiotii wazazi wao wasio na shukrani, wasio safi wasio wapenda wakwao wasio takakufanya suluhu wasingiziaji wasiojizuia wakali wasio penda mema, wasaliti wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu wenye mfano wa utaua lakini wakikana nguvu zake hao nao ujiepushe nao."

Elimu itaongezeka na watu watasafiri huku na kule. hi ni ishara ya siku za mwisho. Imeandikwa, Danieli 12:4 "Lakini wewe Ee Danieli yafunge maneno haya ukatie mhuri kitabu hata wakati wa mwisho wengi wataenda mbio huku na huko na maarifa ya taongezeka."

Je! Bibilia yaonyesha ishara gani za siku za mwisho? Imeandikwa, Luka 21:25-26 "Tena kutakua na ishara katika jua na mwezi na nyota na katika nchi dhiki ya mataifa wakishangaa kwa uvumi wa bahari na msukosuko wake watu wakivunjika mioyo kwa hofu na kutazaia mambo yatakayoupata ulimwengu kwa kuwa nguvu za mbinguni zitatikisika."

Watu wataongea kuhusu amani hi ni ishara ya siku za mwisho. Imeandikwa, 1Wathesalonike 5:2-3 "Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile wivi ajavyo usiku wakati wasemapo kuna amani na usalama ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba wala hakika hawataokolewa."

Je watu wafanyaje wakati mambo haya yanapo endelea? Imeandikwa, Mathayo 24:42-44 "Kesheni basi kwa maana hajui nisiku gani atakayokuja Bwana wenu lakini fahamuni neno hili; kama mwenye nyumba angalijua ile zamu mwivi atakayokuja angalikesha asingeliasha nyumba yake kuvunjwa. Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari kwa kuwa katika saa msiyo dhani mwana wa Adamu yuaja."