Home / Masomo ya Biblia / Kutongozana

Kutongozana

Je tu watongoze watu waaina gani? Imeandikwa 2Timotheo 2:22 "Lakini zikimbie tama za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi."

Sivema kumtongoza mtu asiye mwamini Mungu. Imeandikwa, 2Wakorintho 6:14-15 "Msifungwe nira pamoja na wasio amini kwa jinsi isivyo sawasawa kwa maan apana urafiki gani kati ya haki na uasi? tena pana shirika gani ya Kristo na Beliari au yeye aaminiye ana sehemu gani paomaja na asiyeamini?. Amosi 3:3 yasema "Je! watu wawili waweza kutembea pamoja, wasipokuwa wamepatana?".

Usimtongoze mtu anayesema kuwa ni mkristo lakini matendo yeke ni tofauti. Imeandikwa 1Wakorintho 5:11 "Lakini, mambo yalivyo, naliwaandikia kwamba msichangamane na mtu aitwaye ndugu, akiwa ni mzinzi au mwenyekutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyanga'anyi mtu wa namna hii msimkubali hata kula naye."

Usifanye urafiki na watu wenye hasira. Imeandikwa, Mithali 22:24 "Usifanye urafiki na mtu mwenye hasira nyingi, wala usiende na mtu mwenye ghadhabu nyingi."

Usimtongoze mkristo hafifu. Imeandikwa, 2Timotheo 3:6 "Kwa maana katika hao wamo wale wajiingizao katika nyumba za watu na kuchukua mateka wanawake wajinga wenye mizigo ya dhambi walio chukuliwa na tama za namna nyingi."

Uzuri wa ndani wafaa zaidi. Imeandikwa, 1Petro 3:4 "Bali kuwe utu wa moyoni usioonekana katika mambo yasiyoharibika yani roho ya upole na utulivu, iliyo ya dhamani kuu mbele za Bwana."
Tongoza mtu aliye na tabia njema. Imeandikwa Warumi 15:5-6 "Na Mungu mwenye saburi na faraja awajalie kunai mamoja ninyi kwa ninyi kwa mfano wa Kristo Yesu, ili kwa moyo mmoja na kwa kinywa kimoja mpate kumtukuza Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo."

Kuwa na urafiki na mtu ambaye atakusaidia katika maisha yako. Imeandikwa, Wafilipi 2:1-2 "Basi ikiwapo faraja yo yote katika Kristo yakiwapo matulizo yo yote ya mapenzi ukiwapo ushirika wo wote wa Roho ikiwapo huruma yo yote na rehema, ijalizeni furaha yangu ili mwe na nia moja mwenye mapenzi mamoja mwenye roho moja mkinia mamoja."

Unapotongoza usiwaache watu wengine au marafiki wako. Imeadikwa, Wafilipi 2:4 "Kila mtu asiangaliye mambo yake mwenyewe bali kila mtu aangalie mambo ya wengine."

Wacha urafiki ukuwe hatu kwa hatua. Imeandikwa, 2Petro 1:6-7 "Na katika maarifa yenu kiasi, na katika kiasi chenu saburi, na katika saburi yenu utauwa, na katika utauwa wenu upendano wa ndugu na katika upendano wa ndugu, upendo."

Tuepukane na nini wakati wa kutongozana?. Imeandikwa, Warumi 13:13 "Kama ilivyohusika na mchana na tuenende kwa adabu si kwa ulafi na ulevi si kwa ufisadi na uasherati si kwa ugomvi na wivu."

Tusifanye mapenzi ya kimwili wakati tunapo tongozana. Imeandikwa, 1Wakorintho 6:13, 18 "Vyakula ni vya tumbo na tubo ni kwa vyakula lakini Mungu atavitiwesha vyote viwili tumbo na vyakula lakini mwili si kwa zinaa bali ni kwa Bwana naye Bwana ni kwa mwili, ikimbieni zinaa..."
Jiweke safi. Imeandikwa, 1Yohana 3:3 "Na kila mwenye matumaini haya katika yeye hujitakasa kama yeye alivyo mtakatifu."

Tusijiumize, tama za mwili tuziweke kwake Kristo. Imeandikwa, 1Wathesalonike 4:3-5 "Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kutakaswa kwenu, mwepukane na uasherati, kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima si katika hali ya tama mbaya kama mataifa wasio mjua Mungu."

Je kama umefanya mapenzi nje ya ndoa ufanye nini?.
Kwanza jua dhambi yako na ukubali kuwa umefanya dhambi. Imeandikwa Zaburi 51:2-4 "Unioshe kabisa na uovu wangu unitakase dhambi zangu maana nimejua mimi makosa yangu na dhambi yangu imbele yangu daima nimekutenda dhambi wewe peke yako na kufanya maovu mbele za macho yako wewe ujulikane kuwa una haki unenapo na kuwa safi utoapo hukumu."

Kubali yakuwa Mungu amekusamehe dhambi zako. Imeandikwa, Zaburi 32:1-6 "Heri aliyesamehewa dhambi, na kusitiriwa makosa yake. Heri Bwana asiyemhesabia upotovu ambaye rohoni mwake hamna hila. Nilipo nyamaza mifupa yangu ilichakaa kwa kuugua kwangu machana kutwa. kwa maana mchana na usiku mkono wangu ulinilemea jasho langu likanikauka hata niwaka kama nchi kavu wakati wa kaskazi nalikujulisha dhambi yangu wala sikuufisha upotovu wangu nalisema nitayakiri maasi yangu kwa Bwana, nawe ukanisamehe upotovu wa dhambi yangu. Kwa hiyo kila mtu mtauwa akuombe wakati uanapopatikana haki maji makuu yafurikapo hayatamfikia yeye."

Mungu atakupatia mapenzi. Imeandikwa, Mwanzo 2:18 "Bwana Mungu akasema sivema huyo mtu awepekeyake nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye."

Uliza Mungu mpenzi wako. Imeandikwa, Mithali 19:14 "Nyumba na mali ni uridhi apatao mtu kwa babaye; bali mke mweenye busara, mtu hupewa na Bwana."

Mungu atakupa kilicho nia ya moyo wako. Imeandikwa, Zaburi 37:4 na Mathayo 6:8 "Nawe utajifurahisha kwa Bwana naye atakupa haja za moyo wako" "Basi msifanane na hao; maana Baba yenu mnayohitaji kabla ninyi hamjamwomba."